Gospel Global Ambwene Mwasongwe – Picha ya Pili

Ambwene Mwasongwe – Picha ya Pili

Download Picha ya Pili Mp3 by

The African Christian music minister drops a powerful song alongside its visuals, as this song is titled “Picha ya Pili“. You'll see praising God on this song with joy.

Get AUdio Mp3, Stream, Share & stay graced

DOWNLOAD HERE

DOWNLOAD MORE AMBWENE MWASONGWE SONGS HERE

Lyrics: Picha ya Pili by

Verse 1
Yahitaji macho ya moyo, kuona picha ya pili.
Yahitaji sikio la ndani, kusikia sauti ya moyo.

Nimeona chozi likitiririka, kwenye uso unaocheka.
Nimesikia sauti ya kuugua, katikati ya kigelegele.

Nimeona watu wakienda, kuwaona wahitaji, ila wamebeba kamera uuuh! kuuonyesha ulimwengu.

Yatima nao wajane, mbele ya kamera, hushukuru kwa kutabasamu.
Ila wakibaki peke yao na Mungu hulia kwa kuugua.

Sababu ya uyatima, sababu ya ujane, ni kama twadhalilishwa,. HAWAJUI size ya kiatu hiki namna kinavyobana, Hawajui twaumia.

Chorus 1
Ni Yesu tu, Ni Yesu, Anayeletaga faraja ya moyo kwa aliyeumizwa na kuvunjwa vunjwa bila matangazo… (wewe Yesu u mwema kwetu yooh!..)

Ni Yesu tu ,ni Yesu anayetoaga neno la faraja la moyo, liwe hadharani au la sirini wala haliumizi.

(Ni wewe ufanyaje kwa kutufikiria utu wetu)

Ni yesuuu tu ni Yesu anayetoaga Neno la Faraja Liwe hadharani au la sirini wala Haliumizi

Verse 2
Nilimwona mama analia, mtoto wake kawa teja, anavuja mate mtaani, wenzake wanamcheka.

Wanapiga picha naye wanafanya self wanapost wanacheka.
Wanainjoi wanatafuta views hawajui maumivu ya mzazi.

Kicha kwa mwenzako anachekesha sana, akiwa kwako anauma.
Mlemavu kwa jirani anaburudisha, akiwa kwako anauma.

Niliona wazazi wanalia eeeh! malezi yamewashinda, wamejitahidi sana kusema, watoto hawasikii.

Wanasikia mtaani wanasemwa vibaya, bado hawakati tamaa.
Hata kama ni mwizi, hata kama malaya, ni mtoto wangu hakati tamaa.

Chorus 2
Ni Yesu tu, Ni Yesu asiyewatupa tusiowajali, tunaowasema tuliowachoka na kuwadharau. (eeheee)

Ni Yesu tu Ni Yesu anayeletaga jibu la maswali kwa waliochoka, wenye utata na waliokwama (eeeheee!)

Ni Yesu tu Ni Yesu anayeletaga jibu la maisha kwa waliochoka, wenye maswali, na wenye utata. (Bwana nakuombaaa)

Verse 3
Naomba wakumbuke, tuliowachoka, tunaowasema, tunaowadharau. Bwana warehemu ni watoto na utusamehe.

Samehe makosa Yetu samehe raha yetu, tumefurahiii tukadhani tumefanya kwa ajili yao kumbe kwa ajili yetu.

Samehe Bwana kuwatangaza wao bila kujali utu.

Ni Yesuuuu Ni Yesuuu Ni Yesuuu oooh! Ni Yesuuuu Ni Yesuuu, Ni Yesuuuu, Ni Yesuuuu uuu

Comment below with your feedback and thoughts on this post.